COSTA RICA YAPETA ROBO FAINALI KOMBE LA DUNIA KWA MIKWAJU YA PENATI 5-3 DHIDI YA UGIRIKI



COSTA RICA YAPETA ROBO FAINALI KOMBE LA DUNIA KWA MIKWAJU YA PENATI 5-3 DHIDI YA UGIRIKI

COSTA Rica wamefanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali ya kombe la dunia kwa kuifunga Ugiriki kwa mikwaju ya penati 5-3 baada ya dakika za kawaida na za nyogeza 30 kumalizika kwa sare ya bao 1-1.Hata hivyo kocha wa Ugiriki,  Fernando Santos alitolewa kwenye benchi kwa kuoneshwa kadi nyekundu kutokana na kumzonga mwamuzi katika mchezo huo ulioenda hatua ya penati.
Sokratis (kushoto) akifunga bao la kusawazisha dakika za lala salama 
 
Costa Rica walilazimika kucheza pungufu baada ya mchezaji wake Oscar Duarte kutolewa nje kwa kadi nyekundu mnamo dakika ya 67 kufuatia kadi mbili za njano.

Kikosi cha Costa Rica: Navas, Gamboa (Acosta 77), Duarte, Gonzalez, Umana, Diaz, Ruiz, Borges, Tejeda (Cubero 66), Bolanos (Brenes 83), Campbell.
Wachezaji wa akiba: Pemberton, Myrie, Barrantes, Francis, Granados, Miller, Calvo, Urena, Cambronero.
Kadi ya njano: Duarte, Tejeda, Granados, Ruiz, Navas.
Kadi nyekundu: Duarte.
GMfungaji wa goli: Ruiz 52.
 
Kikosi cha Ugiriki: Karnezis, Torosidis, Manolas, Papastathopoulos, Holebas, Karagounis, Salpingidis (Gekas 69), Maniatis (Katsouranis 78), Christodoulopoulos, Samaris (Mitroglou 58), Samaras. Subs: Glykos, Tzavelas, Moras, Tziolis, Kone, Mitroglou, Vyntra, Fetfatzidis, Tachtsidis, Kapino.
Booked: Samaris, Maonlas.
Mfungaji wa Goli: Sokrats 90+1 dakika moja nyongeza.
Mwamuzi: Benjamin Williams (Australia)


Comments