MASHUJAA BAND MWISHO WA UBISHI …wafunika Letasi Lounge ...pata picha 22



MASHUJAA BAND MWISHO WA UBISHI …wafunika Letasi Lounge ...pata picha 22
MASHUJAA BAND MWISHO WA UBISHI …wafunika Letasi Lounge            ...pata picha 22

ILIKUWA ni kama onyesho la kuwatoa shaka wale wote wenye mashaka na tuzo zao tatu za Kilimanjaro Tanzania Music Awards. Mashujaa Band wakaangusha show ya kutakata ndani ya Letasi Lounge.

Lilikuwa ni onyesho la kushukukuru na kupongezana kwa bendi hiyo kutwaa tuzo za Kili ikiwemo ile kubwa ya bendi bora ya muziki wa dansi.

Chaz Baba, Jado FFU, Ferguson, Pasyaa na Ferguson wakatengeneza safi ya hatari ya 'ushambuliaji' huku mpiga kinanda Fredy Mazaka, mpiga tumba Dulla Ngoma, mpiga drum Sele Kadance na mpiga solo Amos Nabii na wapiga vyombo wengine wakiujaza muziki mnene na kuufanya ukumbi urindime kwa burudani ya aina yake.

Ni moja ya show ambayo Mashujaa walijitahidi kuitendea haki kila idara kuanzia wacheza show, waimbaji hadi wapiga vyombo. Hadi onyesho linamalizika saa 9.27 za usiku kila mtu alikuwa amezuuzika na roho yake.

Unaweza kusema sentesi moja tu – Mashujaa mwisho wa ubishi.

 Wacheza show wakifanya yao
 Pasyaa, Chaz Baba na Jado wakituma masauti
 Chaz Baba akishambulia jukwaa
 Pasyaa akiwajibika jukwaani
 Jado FFU
 Hatari tupu!
 Rapa Ferguson akitupia rap zake
 Ferguson akiendelea kuwashika
 Sauti ya Radi alitesa ile mbaya
 Sauti ya Radi akifanya makamuzi
 Ni mashambulizi kwa kwenda mbele
 Mkurugenzi Masoko wa Mashujaa Max Luhanga akitoa shukran
 Max Luhanga akiendelea kutoa machache
 Fred Mazaka balaa sana katika kinanda
 Chokoraa (kulia) akiteta na Papaa Maisha na Mzee Mbizo
 Wacheza show wakifanya yao
 No comment ...Sweet Baby hugo
 Ferguson na dansa Super K
 Chaz Baba alipohamia kwenye drum
 Suzy na Ben wakali wa Weekend Bonanza ya Clouds FM
 Mathew Kiongozi (kushoto) na Kisanola
 



Comments