KALUNDE BAND TISHA SANA …wapiga bonge la show kuwasindikiza Mashujaa Band Letasi Lounge …pata picha kibaoooo!



KALUNDE BAND TISHA SANA …wapiga bonge la show kuwasindikiza Mashujaa Band Letasi Lounge …pata picha kibaoooo!
KALUNDE BAND TISHA SANA …wapiga bonge la show            kuwasindikiza Mashujaa Band Letasi Lounge …pata picha            kibaoooo!

KUNA bendi hazina makuu wala kelele lakini ukikutana nao jukwaani utazima zako. Mojawapo ni Kalunde Band.

Kalunde wamepiga bonge la show katika onyesho maalum la Mashujaa Band hapa Letasi Longe, Victoria Jijini Dar es Salaam.

Ni onyesho la kupongezana kwa ushindi wa tuzo tatu za Kili Music Awards ambapo Kalunde wamekuja kama wasindikizaji.

Jamaa wanapiga mziki wa dunia yote, ukitaka copy za kila kona utakoma, ukiskia nyimbo zao wenyewe utapigwa na butwaa. Ni bendi ya watu wachache yenye watu wasiozidi 16 lakini wanashambulia kama mchwa.

Moja ya zawadi nzuri ya Kalunde Band kwenye onyesho hili ilikuwa ni pale walipopiga wimbo Solemba ulioimbwa na Msondo Ngoma miaka ya 80 utunzi wake marehemu Nico Zengekala.  Kalunde Waliutendea haki sana wimbo huu ilikuwa ni kama vile Zengekala karejea duniani.

Utawapenda pia walivyo nadhifu jukwaani. Ni aina ya bendi ambayo hutachoka kuitazama.

Kalunde wameshuka jukwaani na kuwapisha Mashujaa Band ambao nao wamepanda na moto mkali. Kama ndo kwanza uko njiani bado hujachelewa.

Mwimbaji Bijah Valentino
Mwimbaji Bijou Hamad "Mvinyo Mvinyo jana na leo"
 Kalonda Kapizo akipapasa kinanda 
Majuto Athuman akikung'uta bass
Rajab, hila John, Bijou Hamad na Bijah Valentino
Deborah Nyangi
 Deborah Nyangi na Shila John
Said Mdoe akiwa na Sauda Mwilima wa Star TV
 Deo Mwanambilimbi (kushoto) na Said Mdoe
Mwimbaji Bijah Valentino
Suzy Baltazary Clouds FM alijitosa ukumbini mapema kabisa 
Kutoka kushoto ni Deo Mwanambilimbi, Bijah Shila na Bijou
Deo Mwanambilimbi akifanya yake
 Kutoka kushoto: Kim mwaadaji wa kipindi cha Afro Dance Channel 10, Deo Muta Mwanatanga, Martin Sospeter, Sunday Mwakanosya, Mwani Nyangasa
Mwandishi Asha Said (kulia) akiwa na mumewe
Bijou na Zomboko wa Radio One wakiimba wimbo Solemba
Meneja wa Mashujaa Martin Sospeter akiwa na Mwenyekiti wa mtandao wa Bongo Dansi, Mathew Kiongozi

 

 



Comments