EVRA BADO YUPO YUPO MAN UNITED, ASAINI MKATABA MPYA WA KUBAKI OLD TRAFFORD




EVRA BADO YUPO YUPO MAN UNITED, ASAINI MKATABA MPYA WA KUBAKI OLD TRAFFORD

Staying put: Patrice Evra has extended his contract                at Manchester United for one year

PATRICE Evra amemaliza utata wa hatma yake Old Trafford kwa kusaini mkata mpya wa mwaka mmoja kuendelea kuichezea Manchester United.

Nyota huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 33, angekuwa huru mwezi ujao baada ya mkataba wake wa awali kufikia ukingoni.

Ujio unaotarajiwa wa beki Luke Shaw mwenye thamani ya pauni milioni 27, ulitarajiwa kumsafishia Evra njia ya kutimka Manchester United.

Lakini Evra ambaye alikuwa akihusishwa na Inter Milan, Juventus, Paris Saint-Germain, amewashangaza wengi kwa kuamua kurefusha maisha yake ndani ya United kwa msimu wa kumi.



Comments