CRISTIANO RONALDO NA PENALTI TATA YA LIONEL MESSI



CRISTIANO RONALDO NA PENALTI TATA YA LIONEL MESSI
Ronaldo reveaked last            month that he would be open to a move to America in the            future
STAA wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo, amedai kuwa anajua ni kwanini Lionel Messi aliamua kupiga penalti kwa kumpasia Luis Suarez aliyefunga katika mechi ya La Liga dhidi ya Celta Vigo Jumapili iliyopita, lakini amekataa kuweka wazi kwa vyombo vya habari.

Ronaldo alifumba fumbo hilo katika mkutano na waandishi wa habari kuelekea mechi ya awali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya 16 bora, alipoulizwa kuhusu 'pasi ya penalti ya Messi kwa Suarez' iliyotawala vyombo vya habari.

"Najua kwanini alifanya hivi, lakini sina cha ziada cha kuongeza," alisema Ronaldo mwenye umri wa miaka 31 na kuwaacha wanahabari 'kwenye mataa' wakihangaika kujiuliza alichomaanisha.

Katika kutafuta alichomaanisha Ronaldo, baadhi waliona ni katika kuonyesha heshima kwagwiji Johan Cruyff, ambaye alifanyatukio kama hilo enzi zake akiichezea Ajax mwaka 1982, wakati wengine wanadhani Messi alikuwa akimsaidia Suarez kumkimbia Ronaldo katika mbio za kuwania tuzo ya mfungaji bora wa La Liga - Pichichi.

Pasi hiyo ya penalti katika mechi waliyoshinda 6-1 ilimfanya Suarez kukamilisha 'hat-trick' na kufikisha mabao 23 mbele ya Ronaldo aliyebaki na mabao 21. Messi ana mabao 13 katika msimamo huo.


Comments